Imefundishwa na
Stephen Armstrong
Imefundishwa na
Stephen ArmstrongTumekamilisha hukumu sita za kwanza ambazo Yesu alileta duniani mwanzoni mwa Dhiki ya miaka saba
Kabla hatujaelekea kwenye wimbi linalofuata la hukumu, hebu tuangalie tena ratiba yetu kwa muda mfupi
Kwanza, tunakumbuka kwamba Ufunuo 6-19 inasimulia hadithi ya miaka saba ya mwisho ya miaka saba ya Danieli.
Pia inajulikana kama wakati wa shida za Yakobo au Dhiki duniani
Ni wakati wa hukumu ulioahidiwa kwa Israeli katika Agano la Kale, na kitabu cha Ufunuo kinaelezea jinsi unavyotimia
Ishara hizo ni pamoja na vita vya dunia, matetemeko ya ardhi na njaa
Na ishara hizi zingeendelea kama maumivu ya kujifungua, Yesu alisema
Kisha katika wiki mbili zilizopita tumeingia katika wimbi la kwanza la hukumu katika Dhiki yenyewe
Yesu alipovunja muhuri mmoj kwenye hati ya umiliki wa Israeli na dunia, matukio yalianza kujitokeza duniani.
Mihuri minne ya kwanza ilianzisha kufunuliwa kwa Mpinga Kristo duniani
Anapopaa hadi kwenye mamlaka na nguvu zaidi, anaanzisha vita vya dunia vinavyosababisha vifo na uharibifu mkubwa
Na matokeo yake yakawa kwamba robo ya idadi ya watu wa dunia—takribani watu bilioni 2—walikufa.
Lakini kulikuwa na pendekezo kwamba nchi ya Israeli inaokolewa kutokana na majanga haya ya awali.
Na hilo linaonekana kuhusishwa na matukio ya Sura ya 7 na kuvunjwa kwa muhuri wa tano.
Katika Sura ya 7 tunajifunza kwamba hata kabla Mpinga Kristo hajaanza kutawala, Bwana yuko kazini akiwaandaa watu 144,000.
Anawaleta wanaume 144,000 Wayahudi kwenye imani ili waweze kumtumikia katika kuufikia ulimwengu kwa injili
Kwa hiyo, hata wakati Bwana analeta wimbi baada ya wimbi la hukumu juu ya dunia, pia analeta rehema kwa mamilioni ya watu.
Mwishoni mwa Sura ya 7, Yohana anaona matokeo ya watu hawa wakifanya kazi: idadi isiyohesabika ya waumini kutoka kila mahali duniani
Wapo Mbinguni jambo ambalo halionyeshi tu mafanikio makubwa ya wale 144,000 bali pia lilionyesha kwamba waliuawa kishahidi.
Muhuri wa tano ulifunua roho za waumini hawa Mbinguni wakitafuta kisasi kwa ajili ya vifo vyao.
Hamu ya Mpinga Kristo ya kupigana vita inalingana tu na mateso yake makali kwa waumini wakati huu.
Na hivyo tulijifunza kwamba kuinuka kwa Mpinga Kristo madarakani ndiko kulisababisha vifo vya wasioamini na waumini.
Sura ya 7 ilikatiza simulizi la kitabu cha Ufunuo, lakini kwa kweli matukio ya Sura ya 7 yanaambatana na mwanzo wa Dhiki Kuu
Na matukio haya hayaishi hadi mwisho kabisa wa miaka saba yote.
Katika wakati huu, Yohana anapewa muhtasari wa uinjilisti wa Dhiki ili aweze kutia moyo kizazi hicho kijacho
Waumini katika wakati wa Dhiki wanaweza kusoma sura hii na kutambua kwamba kuuawa kishahidi si jambo la kuogopa
Ni mpango wa Mungu na kisasi kitakuja hatimaye
Nadhani sura hii itakuwa sura muhimu kwa waumini wakati wa Dhiki Kuu
Aina ya Zaburi 23 kwa wale wanaovumilia kuzimu ya siku hizo
Hii ni faraja ya kujua kwamba majaribu yatamalizika hivi karibuni au baadaye, na kifo ni njia ya baraka ya kukimbia mateso.
Kisha hatimaye, muhuri wa sita unaashiria mara ya kwanza Bwana analeta uharibifu usio wa kawaida duniani
Jua analitia giza, anaufanya mwezi kuwa mwekundu kama damu, analeta vimondo vinavyonyesha duniani
Na Anaitikisa dunia kwa matetemeko makubwa ya ardhi kiasi kwamba kila mlima na kisiwa huondolewa mahali pake
Kwa mara ya kwanza, wanadamu wanakuja kuelewa kwamba uharibifu wa dunia wanaokabiliana nao unakuja kama matokeo ya Mungu mwenye hasira
Hii inatufikisha kwenye wimbi lijalo la hukumu, linaloitwa hukumu za Baragumu (tarumbeta).
Na kama nilivyoelezea mara ya mwisho, hukumu za tarumbeta saba ni hukumu ya muhuri wa saba
Kwa hiyo Yesu anapofungua muhuri wa saba, anaanzisha mfululizo wa hukumu za ziada
Hivyo kuvunjwa kwa muhuri wa saba kunamaanisha kwamba hukumu zingine za Dhiki zitatokea bila shaka.
Sura ya 8 inaanza na Yesu akivunja muhuri wa saba, ambao unaleta athari kubwa Mbinguni
Yohana anasema kuna kipindi cha ukimya Mbinguni kwa takriban nusu saa
Kipindi hicho cha ukimya kinasisitiza jinsi hukumu zijazo zitakavyokuwa za kushangaza na zenye kina
Kuvunjwa kwa muhuri wa saba kunafungua mfululizo wa hukumu ambazo hatuwezi kuzifikiria kwa kiwango kidogo
Hukumu za tarumbeta na bakuli ni kilele cha yote ambayo manabii wametabiri
Na humaliza kila hadithi ya wakati wetu na kusababisha mwanzo mpya kwa kila mtu na kila kitu
Na kama vile kujifungua mtoto, mwanzo wa enzi hiyo mpya huja kupitia kipindi kichungu cha majaribu
Kwa hiyo Mbingu yote inakaa kimya kwa muda, labda kwa mara ya kwanza tangu Mungu alipoumba mahali hapo kwa ajili yake na kwa ajili ya mahakama yake.
Msemo "kama nusu saa" ni jambo la kushangaza kutokana na kutoeleweka kwake kwa usahihi.
Tunajua neno la Mungu huwa sahihi kila wakati na kila neno limekusudiwa, kwa nini Yohana hapa hana uwazi sana?
Labda hakuwa na kifaa cha mwendo wa jua kwenye mkono wake ili kufuatilia muda kwa usahihi zaidi.
Lakini nadhani kutokuwa sahihi ni kwa makusudi ili kuepuka kutuongoza kwenye njia isiyo sahihi katika tafsiri yetu.
Kama Yohana angeandika “kulikuwa na ukimya kwa dakika 30,” tungetumia muda wetu kujaribu kuelewa umuhimu wa 30
Lakini hiyo haikuwa hoja, kwa hiyo aliiacha ikiwa wazi ili tuzingalie ukweli tu kwamba kile kinachokuja hakitakuwa na kifani, bali kitakuwa cha kipekee kabisa..
Kisha tunaona malaika saba wakijiandaa kuleta hukumu zinazofuata, na wimbi linalofuata la hukumu lina mtindo wa kipekee.
Hukumu za tarumbeta zimegawanywa kati ya kuathiri dunia halisi na miili halisi ya wanadamu
Tatu za kwanza zitaleta uharibifu duniani (au kilichobaki) ili maisha yazidi kuwa magumu
Huku tatu za pili zikifanya maisha kuwa magumu sana kwa kila mtu bila kujali anaishi sehemu gani ya dunia.
Hukumu hizo tatu za mwisho juu ya mwili wa kila mtu ni mbaya sana kiasi kwamba zinaitwa hukumu za "ole".
Neno "ole" ni neno la Biblia linalomaanisha hukumu ya milele, na kwa hiyo hukumu hizi ni hakikisho la hukumu ya milele
Tutaelezea hili zaidi tutakapofikia hukumu hizo
Wakati huo huo, kabla ya hukumu kuanza, Mungu hupokea maombi ya watakatifu kama inavyoonyeshwa na uvumba mbele ya Kiti cha Enzi.
Tunaweza kudhani maombi haya ni ya waumini wanaomba ulinzi, kinga, na unafuu kutokana na yale wanayopitia.
Na kama tutakavyoona tunapoangalia hukumu, hasa hukumu za ole, Bwana husikia maombi ya watakatifu wake
Hatimaye, hukumu hizi zinatangazwa kwa tarumbeta, kwa sababu zinatumika kama maonyo ya mwisho ya enzi
Seti ya kwanza ya hukumu, hukumu za muhuri, ziliweka msingi wa miaka saba
Hazikuonekana kama zilitoka Mbinguni, angalau mwanzoni
Na kwa kweli, hukumu ya muhuri wa sita pekee ndiyo iliyomsaidia Mungu kuwajulisha watu wote duniani kwamba alikuwa akifanya kazi katika mambo haya.
Lakini sasa kwa kuwa siri imefunuliwa, dunia imepewa onyo kwamba mwisho uko karibu.
Na tunapokaribia katikati ya Dhiki, Bwana anatangaza mwisho huo kwa hukumu hizi za tarumbeta
Kila hukumu ni kama mlio wa tarumbeta ya onyo ikikumbusha ulimwengu kwamba wakati unaisha
Hukumu sita za tarumbeta zote hutokea wakati wa nusu ya kwanza ya Dhiki, ambayo tutaiona wazi zaidi tunapoingia katikati ya Dhiki.
Hilo litaacha wimbi moja tu la hukumu, hukumu za bakuli
Hukumu hizi huja karibia mwisho wa nusu ya pili ya Dhiki Kuu na zinamaliza enzi hii.
Kwa hiyo hukumu hizi za tarumbeta zinawakilisha nafasi ya mwisho kwa ulimwengu kuja kwenye imani kabla ya mabaya zaidi kuja.
Tutajifunza ratiba hii kwa undani zaidi baadaye
Kabla tarumbeta ya kwanza haijapigwa, kuna maandalizi zaidi katika mfumo wa mfululizo wa majanga ya uharibifu duniani.
Mfululizo mzima wa hukumu za tarumbeta hutanguliwa na maonyesho mbinguni na tetemeko lingine la ardhi
Tunakumbuka kutoka kwewnye mafundisho/Hotuba ya Mizeituni kwamba matetemeko ya ardhi yataendelea kuwa ishara ya onyo la hukumu ijayo
Yataendelea kuongezeka kwa nguvu na muda, na hapa tunaona moja kati ya ishara hizo tena.
Na sasa tarumbeta zinaanza kupigwa na hukumu zinafuata
Baragumu ya kwanza ilipopigwa, theluthi moja ya dunia iliteketea kwa moto wa mawe, na damu.
Hii ni hukumu isiyo ya kawaida na inatukumbusha hukumu dhidi ya Misri katika kitabu cha Kutoka
Kufanana huku kati ya hukumu ya tarumbeta ya kwanza na pigo la Kutoka si kwa bahati tu, una maana ya kipekee.
Katika hukumu zote za tarumbeta tutaona ulinganifu mdogo kati ya Kutoka na Dhiki Kuu kwa sababu moja inatambulisha ile nyingine.
Na katika umbo la kawaida la Kibiblia, hukumu hizo za awali zilikuwa toleo dogo la utimilifu mkubwa zaidi ulioonekana katika Dhiki
Katika simulizi ya Kutoka, Israeli ilikuwa utumwani kwa taifa la kigeni
Na katika siku hizi za mwisho Israeli itakuwa katika utumwa wa adui na dhambi
Katika Kutoka, Bwana aliwatoa Israeli kutoka kwenye utumwa wa kiduniani kupitia mfululizo wa hukumu zisizo za kawaida
Na katika Dhiki Kuu, atawakomboa Israeli kutoka utumwa wa kiroho kupitia mfululizo wa hukumu kubwa zaidi
Katika Kutoka, uhuru wa Israeli uliwezeshwa na Sheria, kama ilivyobinafsishwa na Musa akiwaongoza watu jangwani
Na katika Dhiki Kuu, watu watarudi kwanza kwenye Sheria ili kuabudu hekaluni, jambo ambalo litawaandaa kumpokea Masihi.
Na katika Kutoka, watu hatimaye walipata njia yao ya kuelekea Nchi ya Ahadi wakiongozwa na Yoshua (Yeshua)
Na mwisho wa Dhiki Kuu, watu wa Israeli hatimaye wataingia katika Ufalme unaoongozwa na Yeshua, Masihi wao.
Kwa hiyo tukielekea kwenye hukumu ya kwanza, Yohana anatuambia kwamba theluthi moja ya dunia itateketea, lakini "theluthi" inamaanisha nini?
Je, tuseme ni eneo moja linaloungana la duniana kuacha theluthi mbili zingine, au je, theluthi hiyo imesambazwa (imegawanywa) sawasawa kote duniani?
Tunapoendelea zaidi katika hukumu za Ufunuo, jibu linakuwa dhahiri
Hii ni sehemu moja linaloungana la dunia; theluthi moja ya uso wa dunia imeungua na imekuwa isiyoweza kukaliwa na watu.
Hii ni hukumu ya kwanza katika mfululizo wa hukumu zinazoangamiza dunia hadi sehemu ndogo tu iliyobaki
Sababu ya hilo inakuwa wazi zaidi tunapoendelea mbele katika hukumu hizi na katika matukio ya Sura ya 17 na 18.
Kwa mfano, hukumu inayofuata ya Baragumu inaendelea na mtindo huo
Yohana anaelezea kuona kitu kama mlima mkubwa ukiwaka moto ukianguka baharini
Hatuwezi kujua "mlima huu mkubwa" utakuwa nini na baadhi wamekisia kwamba ni kimondo kikubwa kinachoanguka
Au labda ni matokeo ya volkano kubwa ya baharini
Lakini ni sawa kudhani kwamba kama ingekuwa volkano au kimondo, basi Yohana angetambua mojawapo ya mambo hayo
Lakini kwa jinsi Yohana anavyoelezea, tunapaswa kudhani ni kitu tofauti kabisa na kisicho cha kawaida
Yohana anasema athari ya mlima kugonga bahari ni maji kugeuka kuwa damu
Lakini volkano na vimondo havibadilishi maji kuwa damu, hili ni wazi
Hii ni hukumu nyingine inayotukumbusha simulizi ya Kutoka, isipokuwa kwamba ukubwa wake ni mkubwa zaidi kuliko tu Mto Naili kugeuka kuwa damu.
Na tunajua kwamba Yohana anazungumzia damu kihalisi kwa sababu athari yake ni sawa na kile kilichotokea kwa Mto Naili.
Utakumbuka kwamba Mto Naili ulipogeuka kuwa damu, ilisababisha samaki kuangamia, na hicho ndicho tulichotegemea kuona kikitokea hapa pia.
Na vivyo hivyo, Yohana anasema bahari kugeuka kuwa damu husababisha viumbe vyote vya baharini kufa.
Na meli zilizokuwa kwenye maji hayo pia ziliharibika na kupotea
Maelezo hayo yanaangazia sana uhalisia wa hukumu hii kwa sababu ni halisi kiulimwengu.
Uzito maalum wa damu ni mkubwa kuliko maji, na matokeo yake hutoa uwezo mkubwa wa kuelea (kupanda juu zaidi)
Meli iliyokuwa ikielea baharini ingeinuka ghafla juu zaidi pale maji hayo yalipogeuka kuwa damu
Kupanda juu sana kungeifanya meli kuwa na hali tete, bila uimara na kuzama kwa urahisi
Zaidi ya hayo, mifumo ya meli ingechafuliwa na ulaji wa damu kwenye matundu ya hewa na mifumo ya kupoeza.
Angalia tena Yohana anasema hukumu hii iliathiri theluthi moja ya bahari zinazofunika dunia
Na tena, tunahitimisha kwamba eneo lililoathiriwa linalingana na sehemu moja inayoendelea ya bahari
Haiwezekani kabisa kwa theluthi moja tu ya maji kuwa damu, kwani yangetawanyika haraka
Kwa hiyo, njia pekee ya kiutendaji ya hili kutokea ni kama mwili mmoja wa maji sawa na tatu ya maji yote ya dunia ungegeuka kuwa damu.
Hilo linathibitisha tafsiri niliyotoa hapo awali kwamba Bwana anapunguza eneo linaloweza kutumika duniani hatua kwa hatua ili kutoa hoja.
Katika kipindi cha hukumu za Dhiki, Bwana anapunguza mwelekeo wa ulimwengu hadi eneo la Mashariki ya Kati
Matukio ya Dhiki yatafikia kilele chake katika vita itakayotokea katika eneo kati ya Yerusalemu na Babeli
Itakuwa vita kati ya magharibi dhidi ya mashariki, mema dhidi ya mabaya, Yesu dhidi ya Shetani
Kwa hiyo katika kujiandaa kwa vita hivyo vya mwisho, Bwana anaanza kuangamiza uhai wote katika sayari nzima hatua kwa hatua.
Kufikia wakati vita vitakapoanza, Bwana atakuwa ameangamiza sehemu iliyobaki ya dunia
Hakutakuwa na mtu mwingine yeyote na hakuna mahali pengine popote panapofaa, kwa hiyo umakini wote unaelekezwa kwenye vita vya mwisho vya kukomesha Dhiki Kuu
Kwanza, Bwana anateketeza theluthi moja ya ardhi, kisha anageuza theluthi moja ya bahari kuwa damu na viumbe vyote vilivyo ardhini na baharini vinakufa.
Tunajua Israeli na Babeli zinabaki salama na zikiwa na wakazi hadi mwisho kabisa wa Dhiki Kuu.
Kwa hiyo lazima tudhani kwamba Bwana anaanza uharibifu upande wa pili wa sayari na kuendelea kutoka hapo.
Hukumu hizo huchukua ardhi na bahari zaidi hatua kwa hatua hadi Mashariki ya Kati pekee ndiyo inabaki
Cha kufurahisha ni kwamba, eneo la bara lililo moja kwa moja mkabala na Israeli ni Amerika ya Kaskazini na Kusini, na bahari iliyo mkabala na Israeli ni Bahari ya Pasifiki.
na si kwa bahati mbaya, Amerika Kaskazini na Kusini zinawakilisha asilimia 30 kamili ya ardhi yote ya dunia.
Na Bahari ya Pasifiki ni asilimia 30 ya bahari zote duniani.
Kwa hiyo ni busara kudhani kwamba hukumu ya tarumbeta ya kwanza na ya pili huleta mwisho wa maeneo haya duniani.
Kwa hiyo usifanye juhudi nyingi kuokoa sayari…haiwezi kuokolewa
Sasa tunaingia kwenye hukumu ya tarumbeta ya tatu…
Tarumbeta ya tatu inapulizwa na pamoja nayo inakuja hukumu ya tatu na ya mwisho dhidi ya uso wa dunia
Yohana anasema “nyota” kubwa inayowaka moto inaanguka kutoka mbinguni na kuingia katika maji matamu duniani na kuyafanya yawe machungu
Nyota hii ina jina "Pakanga", ambalo halina maana nyingine katika Kigiriki kwa hiyo kwa muktadha tunadhani linamaanisha uchungu
Na katika kujaribu kutafsiri aina ya nyota hapa, tunapaswa kupitia baadhi ya uwezekano
Kwanza, haiwezi kuwa nyota halisi, kwa kuwa jua linalowaka haliwezi kuanguka juu ya Dunia na hakika halingeathiri tu maji safi.
Dunia ingemezwa kabisa na jua lolote linalogusa Dunia
Kama tulivyoona katika hukumu ya muhuri wa sita katika Sura ya 6, nyota hii inaweza kuwa kimondo, kwa kuwa inaanguka kutoka mbinguni na inawaka moto.
Lakini kimondo hakingegeuza maji kuwa machungu tu, wala hakingeweza kugonga theluthi moja ya maji safi yanayozunguka sayari.
Tatu, nyota hii ina jina, ambalo si la kawaida katika Maandiko linapoelezea vitu visivyo na uhai kama vile vimondo.
Ishara inapotajwa katika Maandiko, kwa kawaida huashiria mtu
Ambayo inatuleta kwenye aina ya mwisho ya "nyota" katika Maandiko: uwakilishi wa mfano kwa malaika
Lakini katika Maandiko, malaika wanaweza kuwa na aina mbili za majina
Malaika wanaweza kuwa na majina yanayomtukuza Mungu, kama vile Gabrieli ( mtu wa Mungu ) na Mikaeli ( nani aliye kama Mungu? )
Au malaika wanaweza kuwa na majina yanayopendekeza ufisadi (uharibifu) na asili iliyopotea, kama vile Wormwood au Abadoni (baadaye katika Ufunuo)
Kwa hiyo huyu huenda ni malaika aliyeanguka (pepo) aliyetumwa na Mungu kufanya mapenziyake na athari ya pepo huyu ni kuharibu theluthi moja ya maji safi ya dunia.
Mungu anaweza kutumia mawakala wa pepo kwa madhumuni yake mara kwa mara
Na matumizi Yake ya pepo hapa kuleta hukumu duniani ndiyo ya kwanza katika mtindo unaohusisha hukumu za tarumbeta.
Malaika na pepo watajitokeza zaidi na zaidi katika utekelezaji wa hukumu zitakazofuata
Mada ya "theluthi" inaendelea huku theluthi moja ya jua, mwezi na nyota zikilengwa katika hukumu hii...lakini hii inaweza kuwa ya kutatanisha kidogo mwanzoni.
Inamaanisha nini kwamba theluthi moja ya jua, mwezi na nyota zimetiwa giza?
Je, ina maana kwamba theluthi moja ya vitu hivi huondolewa, au kwamba kila kitu hupunguzwa katika utoaji wa mwanga kwa theluthi moja?
Maelezo ya Yohana yanaonekana kuonyesha tafsiri ya tatu
Yohana anasema kila kitu huangaza kwa theluthi moja pungufu ya mara moja, kwa hiyo taa huzimwa theluthi moja ya mara ambazo kwa kawaida huangaza.
Anasema mchana haungeangaza kwa theluthi moja yake, na usiku haungeangaza kwa theluthi moja yake.
Kwa jumla, hiyo ina maana kwamba dunia inapokea theluthi moja ya nishati pungufu kutoka kwa jua na nyota
Hii ina maana fulani, kwa kuwa mwezi huakisi mwanga wa jua
Kwa hiyo ingawa jua huzima kwa theluthi moja ya siku, pia huzima wakati wa theluthi moja ya siku upande mwingine wa sayari.
Hilo lingesababisha mwezi kuwa mbali kwa wakati mmoja
Kwa hiyo theluthi moja ya usiku na theluthi moja ya mchana ingewakilisha theluthi moja ya siku ya saa ishirini na nne.
Na vivyo hivyo nyota zikiacha kung'aa kwa theluthi moja ya usiku huenda zilipangwa sambamba na mwezi na jua.
Athari ni kuzima kabisa kwa ulimwengu wote kwa theluthi moja ya kila kipindi cha saa 24.
Mbali na sababu dhahiri ya hofu, mabadiliko haya yangesababisha kushuka kwa kasi kwa halijoto duniani
Hii ingekuwa kama hali ya “majira ya baridi ya nyuklia.”
Mazao yangeharibika, vyanzo vya maji vingeganda, mifugo ingekufa
Dunia tayari imeshuhudia robo ya idadi ya watu wakifa kutokana na vita, magonjwa ya mlipuko, na njaa
Na kisha idadi isiyojulikana ya maisha ya ziada yalipotea wakati mabara ya Kaskazini na Kusini mwa Amerika yalipoharibiwa.
Na kisha zaidi walikufa wakati theluthi moja ya bahari na maji safi ilipochafuliwa au kupotea
Na sasa mbingu zinaleta joto na mwanga mdogo duniani na kusababisha vifo vingi zaidi.
Na wale wanaookoka huona maisha kuwa magumu zaidi na zaidi, na kwa ujumla athari yake ni kama kuzimu ndogo duniani.
Jambo kuu ni kwamba kadri dunia inavyozidi kuwa ngumu kwa maisha ya binadamu, watu wote kwa idadi yao duniani wanapaswa kufikiria kuhusu kitakachofuata.
“Wakati huo huo, Mpinga Kristo anaendelea kushambulia na kutawala, hata wakati dunia aliyokuwa akiiitaji inavyozidi kuwa isiyofaa kwa maisha ya binadamu.”
Na wale 144,000 wanaendelea kuileta Injili kwa ulimwengu uliopotea na unaokufa milele tayari kuepuka hukumu
Hatimaye, hukumu za tarumbeta zinasimamishwa kwa muda mfupi ili kutoa onyo lingine kwa dunia
Tai anaruka katikati ya mbingu, Yohana anasema, na neno katikati ya mbingu linahitaji muda wa maelezo
Wayahudi hawakuwa na maneno tofauti ya Kiebrania kwa sehemu hizi tofauti
Anga, anga la juu (nje ya tabaka la hewa la dunia) na chumba cha kiti cha enzi cha Mungu viliitwa kwa neno lile lile la Kiebrania: shamayim linalomaanisha "mbingu"
Kwa hiyo, ili kutofautisha kati ya “mbingu” hizi tatu, Wayahudi waliwaweka namba kuanzia ardhini na kuendelea juu.
Mbingu ya kwanza ni mahali ambapo ndege huruka
Mbingu ya pili au ya kati ni mahali pa sayari na nyota
Na mbingu ya tatu ni mahali ambapo Mungu anakaa
Katika kisa hiki, Yohana anasema kulikuwa na tai akiruka katikati ya mbingu, ambayo inarejelea anga za nje, nje ya angahewa letu.
Ni wazi kwamba tunajua kwamba tai halisi hawawezi kuishi angani
Zaidi ya hayo "tai" huyu anazungumza kwa sauti kubwa kutangaza kwa ulimwengu wote kwamba hukumu zaidi zinakuja
Kwa hiyo neno tai linamaanisha malaika, na Yohana anamwita tai labda kwa sababu anaenda mbele na nyuma, akizunguka kutoa onyo lake
Onyo la "tai" linatangaza kwamba tarumbeta tatu za mwisho zinakuja na zitakuwa ole, ole, ole kwa dunia
Kama nilivyosema hapo awali, hukumu hizi zitaelekezwa kwa miili halisi ya watu badala ya kuelekezwa kwa dunia halisi yenyewe.
Na kama neno "ole" linavyopendekeza, kitakuwa kipindi kibaya zaidi
Itakuwa mbaya sana kwamba hata kifo si njia ya kutoroka kwa wale wanaoteseka
Muundo wa hukumu hizi za maangamizi unafanana na mfumo wa rundo la vitu vinavyoweza kufungamana ndani ya vingine tuliyojadili awali, ambapo hukumu moja inafuata nyingine na ndani yake kuna nyingine, zikijirudia.
Kama vile hukumu ya muhuri wa saba ilivyo hukumu zote za tarumbeta, ndivyo inavyoendelea hapa tena
Hukumu ya tarumbeta ya saba ni hukumu ya mabakuli saba
Kwa hiyo hukumu za Baragumu ya 5, 6 na 7 ndizo hukumu za ole
Hukumu mbili za kwanza ni hukumu mbili za mwisho za Baragumu
Na hukumu za ole ya tatu ni hukumu zote za bakuli zinazomwagwa
Hukumu za ole ya tatu, ambazo ni hukumu za bakuli, ni kama mkusanyiko wa hukumu zote zilizotangulia, zikichanganywa pamoja.
Zaidi ya hayo, maji mengine yanageuka kuwa damu, mashambulizi zaidi kwenye miili ya watu, misukosuko zaidi ya jua, n.k.
Hukumu hizo zitamaliza enzi
Lakini kwa sasa, hebu tuangalie hukumu ya ole wa kwanza
Hukumu hii ya ole inaanza kama vile nne za kwanza zilivyoanza kwa tarumbeta kupigwa na hivyo onyo la tano sasa linaanza na nyota inaanguka kutoka mbinguni hadi duniani.
Muktadha hapa hurahisisha kuona kwamba nyota hapa ni malaika mwingine aliyeanguka, si kimondo au jua linalowaka
Baadaye katika mstari wa 1 Yohana anaielezea nyota hii iliyoanguka kama "yeye"
Na matendo ya "nyota" hii yanaweka wazi kuwa ni mtu, si kitu
Kwa hiyo tena, neno nyota linamaanisha malaika, na malaika anayeanguka chini ni picha ya pepo; malaika mwenye dhambi, aliyeanguka
Baadaye katika mstari wa 11 tunapata jina la pepo huyu, Abadoni au Apolioni
Apolioni inamaanisha mwangamizi kwa Kigiriki, ndiyo maana Yohana anatupa ufafanuzi huo ili tuweze kujua Abadoni anamaanisha nini (kwa Kiebrania)
Kwa hiyo kama nilivyosema hapo awali, jina hasi kama hili lingethibitisha kuwa huyu ni malaika aliyeanguka au pepo aliyeitwa kutumikia makusudi ya Mungu.
Pepo amepewa ufunguo wa shimo lisilo na mwisho, Yohana anasema, na hiyo ina maana kwamba ana ruhusa ya kuwaweka huru wale waliomo shimoni.
Shimo hilo linaelezewa kama lisilo na mwisho na linafikiwa kupitia dunia, kwani hapo ndipo malaika huyu anapotua
Neno la Kigiriki lisilo na mwisho, abussos , linamaanisha shimo la chini kabisa (abyss)
Maneno haya yote yanarejelea mahali pa chini ya dunia, mahali ambapo Biblia inasema ni gereza la roho zisizotii
Neno linalotumika sana katika Agano la Kale kwa mahali hapa ni Sheol au shimo
Kulingana na Luka 16, Sheol ni sehemu mbili, moja kwa ajili ya roho za wasioamini na moja kwa ajili ya roho za watakatifu wa Agano la Kale.
Kabla ya Yesu, Mungu aliwashikilia wote waliokufa hapa: watakatifu katika faraja na wasioamini katika mateso
Baada ya ufufuo wa Bwana, roho za waumini ziliondolewa na kuandamana na Yesu Mbinguni
Lakini roho za wasioamini zilibaki na bado zipo hapo leo, mahali panapoitwa Hadesi au pengine panapojulikana kama shimo.
Lakini Agano Jipya pia linatuambia kwamba mahali hapa kuna kona maalum au gereza ambapo roho za malaika wasiotii hushikiliwa.
Mashetani ambao ni waovu sana wametupwa mahali hapa ili wafungwe kwa muda
Abyss au shimo halishikilii tu roho za wasioamini waliokufa bali pia roho za malaika waasi
Siyo pepo wote wanaoishi shimoni…wengi bado wanazurura huru, lakini baadhi walikuwa wabaya sana kiasi kwamba Mungu aliwaweka kizuizini ili kupunguza ghasia zao.
Sasa umefika wakati wa Bwana kuwaruhusu hawa pepo wabaya zaidi walioanguka kutoka kwenye kifungo chao cha muda.
Pepo huyu mkuu amepewa ruhusa ya kuwaachilia, na inaonekana kwamba Mwangamizi anaweza kuwa si mwingine ila Shetani mwenyewe.
Yeye ndiye bwana wa pepo, kulingana na Mathayo 25
Na ukweli kwamba malaika huyu aliyeanguka anaitwa mwangamizi unaongeza uzito katika tafsiri hiyo.
Mungu humpa pepo huyu, yule aliyepo, ufunguo wa kufungua shimo ili pepo walio ndani waweze kuachiliwa kama mbwa wenye kichaa
Wanatoka shimoni wakiwa wamejaa hasira, wakiwa wamefungwa humo kwa maelfu ya miaka
Bila shaka wana hamu ya kuharibu dunia
Shimo linapofunguliwa, moshi wa mahali hapa unapanda ili kuzuia mwanga wa jua, Yohana anasema
Hii inathibitisha ushuhuda wa Biblia unaoendelea kwamba Kuzimu na shimoni viko moja kwa moja chini ya miguu yetu, katikati ya dunia.
Je, lava inayolipuka kutoka ardhini mara kwa mara inaweza kuhusishwa na shughuli za Kuzimu kwa namna fulani?
Kabla hatujacheka pendekezo hili, kumbuka kwamba wanasayansi hawana uelewa wa kile kilicho chini ya uso wa dunia.
Hatujachunguza zaidi ya maili chache chini ya uso wa dunia
Kulingana na Biblia, shimo au kuzimu (au huitwa Jehanamu) ni mahali halisi pa kuchomwa moto duniani
Ni joto lisiloelezeka na giza kabisa, na sasa giza linatoka nje.
Mara tu shimo lliipofunguliwa, Yohana anaelezea kile anachokiona kikitoka mahali hapa
Anasema anaona "nzige" wakishuka duniani ambao wana nguvu kama ile ya nge waliyopewa.
Yawezekana, mtoaji wa nguvu hiyo ni Mungu, kwa kuwa kutoka kwao kulipangwa na Mungu kama sehemu ya hukumu hii juu ya wanadamu.
Na nguvu zao huja na maagizo na mipaka maalum
Haziwezi kudhuru mimea ya nchi, bali ni watu fulani tu
Hii ni kinyume cha nzige wa kawaida, kwani wadudu wa kweli (nzige) hudhuru mimea tu.
Hawawezi kuchukua uhai wa mtu yeyote, ni kuwatesa tu kwa muda
Na kuna kundi la watu ambao hawawezi kudhuriwa na hukumu hii hata kidogo
Maandiko yanasema Mungu hatawaweka watoto wake kwenye ghadhabu na anatofautisha kati ya wacha Mungu na wasiomcha Mungu katika hukumu zake.
Kwa hiyo wanaume walio na muhuri wa Mungu wametengwa kutokana na shambulio lao, jambo ambalo kwa wazi linawarejelea wale 144,000 waliotajwa katika Sura ya 7.
Na lazima pia iwahusu wale wanaoamini kutokana na wale 144,000.
Hawatakabiliwa na hukumu hii, lakini kwa kuwa hii ni mara ya kwanza kuona ubaguzi, tunahitaji kuutumia kwa uangalifu.
Isipokuwa hii inatumika haswa kwa mashambulizi kwenye mwili wa mtu
Kwa hiyo ni mantiki kudhani kwamba hukumu za awali dhidi ya dunia halisi ziliathiri kila mtu ikiwa ni pamoja na waumini
Lakini sasa kwa kuwa hukumu zinawalenga watu kwa njia mbaya sana, Bwana anafanya tofauti
Bwana amefanya hivi hapo awali alipokuwa akihukumu ulimwengu kwa njia isiyo ya kawaida
Tunajua alimwokoa Nuhu na familia yake kabla ya gharika na alimwokoa Lutu na familia yake kabla ya kiberiti huko Sodoma.
Na katika kisa cha Israeli, Bwana aliwahifadhi wacha Mungu ndani
Yohana anaelezea mateso ambayo mapepo hawa watayaleta, na ni mabaya sana kiasi kwamba ni vigumu kuelewa
Tofauti na hukumu za awali, mapepo haya hayaruhusiwi kuidhuru dunia hata kidogo, kwa sababu sasa shabaha itakuwa mwili wa kila mtu.
Mashetani yatasababisha maumivu makali kwa jumla ya miezi mitano
Yohana anasema mateso yatakuwa kama yale ya kuumwa na ng'e, na kuumwa na ng'e ni jambo linalojulikana kuwa chungu ingawa mara chache husababisha kifo.
Baadhi ya sumu zilizomo kwenye sumu ya nge zina nguvu sana kiasi kwamba hutumika katika tiba ya kemotherapi kuua seli za saratani.
Usumbufu wa mateso haya huongezeka mara nyingi zaidi kwa sababu ya muda wake.
Maumivu ya kuumwa hudumu kwa miezi mitano, na haijulikani wazi ikiwa kuumwa mara moja hudumu kwa kipindi hicho chote au ikiwa kuumwa kunarudiwa bila kukoma.
Hebu fikiria kuishi kwa miezi mitano na ng'e wakitambaa chini ya nguo zako wakikuuma kila mara
Haiwezekani kufikiria athari za kimwili na kisaikolojia za kuvumilia miezi 5 ya mashambulizi kama hayo
Tunajua inachukua miezi mitano, lakini nadhani wale wanaopata adhabu hii hawatajua inachukua muda gani wanapoivumilia.
Wangelazimika kusoma na kuamini Maandiko ili kujua urefu na hivyo kwao inaweza kuonekana kuwa haina mwisho.
Tunapotafakari hatima kama hiyo ya kuumwa bila mwisho, tunaweza kuona jinsi inavyoweza kumfanya mtu afikirie kujiua.
Mtu mwenye akili timamu atakuwa tayari kujiua badala ya kukabiliana na siku nyingine ya maumivu
Na Bwana alitarajia hamu hii, kwa hiyo hukumu ina mgeuko mbaya sana
Chaguo la kufa kwa njia yoyote ile linaondolewa na Mungu katika miezi hii mitano
Yohana anasema katika mstari wa 6 wanadamu hatimaye watatafuta kujiua badala ya kuteseka kupitia hukumu hii lakini Mungu ataizuia kwa njia isiyo ya kawaida.
Inavutia kufikiria jinsi Mungu anavyoweza kutimiza hili
Je, atawafanya watu waishi milele? Kama Superman?
Vipi kama mtu atajitupa kwenye moto au kujilipua kwa bomu? Angeishi vipi?
Wanajikunyata tu kwa maumivu siku nzima bila kupata nafuu na bila nguvu ya kufanya chochote kujidhuru.
Mtu hukabiliana na mateso kiasi gani kabla ya kutamani kifo?
Tutarudi kuchunguza swali hilo, lakini kwanza Yohana anaelezea viumbe hawa
Amekuwa akiwaita ng'e, lakini tayari tulijua hawa hawakuwa ng'e wa kweli
Kwanza, zilitoka mahali pa mashetani na roho zilizokufa
Haijalishi unawachukia vipi ng'e, naweza kukuhakikishia kwamba shimo hilo si chanzo cha ng'e.
Hata hivyo, ninashuku kwamba shimo hilo ndilo chanzo cha mbwa wadogo aina ya poodles...
Pili, wana miiba ambayo si kama ng'e wa kawaida.
Kwa hiyo ni wazi kuna kitu kisicho cha kawaida kuhusu ng'e hawa
Na tunapozingatia maelezo ya Yohana kuwahusu, inakuwa dhahiri kwamba wao si kama ng'e wa kawaida tunaowajua.
Viumbe hawa hawaonekani kama nzige wowote ambao tumewahi kuwaona
Yohana anasema wanaonekana kama farasi walioandaliwa kwa vita, vichwa vyao vikiwa kama vya wanaume, nywele kama za wanawake na meno kama ya simba.
Wanavaa taji ( stephanos ) zinazoonyesha kuwa wana mamlaka katika ulimwengu wa mapepo.
Wana mabawa yanayotoa sauti kubwa na wana mikia kama ng'e, wakiwa na uwezo wa kuwadhuru wanadamu.
Sehemu hii inaelezea wazi kwa nini Yohana alitumia neno ng'e kuelezea viumbe
Mikia yao ndiyo sifa yao kuu na inafanana na ng'e
Lakini kwa ujumla, maelezo haya yanathibitisha kwamba tunaangalia kitu kingine cha ulimwengu
Baadhi wamejaribu kuelezea hili kwa maneno ya kawaida, kama helikopta au kifaa kingine cha kisasa cha vita
Uvumi kama huo si tafsiri sahihi wala hauendani na muktadha
Helikopta za Apache hazitoki shimoni wala hazisababishi maumivu ya miezi 5
Na kwa kuzingatia kiasi cha uharibifu uliofanywa duniani kufikia hatua hii, haiwezekani kwamba vifaa vyovyote vya mitambo bado vinafanya kazi.
Tunahitaji kuona dunia kama magofu, teknolojia imetoweka, hakuna umeme, hakuna maji ya bomba, watu wamegeuka kuwa wazururaji na wakimbizi
Na katikati ya mateso hayo, mapepo haya husababisha mateso makubwa zaidi
Yohana anaelezea kundi la pepo walioachiliwa kutoka shimoni na mwonekano wao ni kitu cha kutisha, kama ng'e
Kujua kwamba wao ni mapepo hujibu tatizo lingine…
Ng'e hawa waliwezaje kumfikia kila mtu duniani (angalau wale ambao hawajatiwa muhuri?)
Kwa mfano, kwa nini mtu hakuweza kujificha kwa mafanikio kutokana na uvamizi?
Jibu ni kwa sababu roho hizi zina uwezo wa kupita kiasi wa kwenda popote bila kuzuiwa na kuta au vizuizi vingine.
Na wana ujuzi na uwezo zaidi ya mwili na damu na wamewezeshwa kutimiza utume huu na Mungu.
Kwa hiyo wanampata kila mtu na kumtesa kila mtu
Tunaweza pia kujiuliza kama watu wanaweza kuona viumbe hawa au hawaonekani
Nadharia yangu ni kwamba viumbe hivi vinaonekana kwa kila mtu, ili chanzo cha hukumu ya maumivu kiwe cha wazi.
Hatimaye, tunapaswa kujiuliza swali la msingi kuhusu hukumu hii: kwa nini Mungu anawaletea wanadamu adhabu kama hiyo? Inatimiza kusudi gani zuri?
Tunaweza hata kujaribiwa kufikiria ilikuwa ya kikatili, hasa kwamba watu hawa wanalazimika kuvumilia mateso haya bila uwezo wa kuyaepuka.
Naam, kama hii ni ukatili, tungeiona rehema kama nini?
Je, Mungu anapaswa kuwaacha wafe? Na kama wangekufa, ni nini kinachofuata kwao?
Wangehama kutoka hali ya mateso ya muda hadi hali ya mateso ya kudumu
Hivyo kwa maana hiyo, kuwatoa kutoka katika hali hizi ni aina ya neema kwao.
Kwa kweli, kipindi hiki cha miezi mitano ni mara ya kwanza na ya pekee katika historia yote ya wanadamu tangu Bustani ambapo kifo hakiwezekani.
Kwa mara ya kwanza tangu mwanzo wa ubinadamu, hakuna mkazi mpya wa Kuzimu kwa miezi mitano
Mungu kwa rehema anazuia kifo kwa kila mtu ili awape waovu kuonja kile kinachokuja baada ya kifo.
Fikiria asili ya hukumu hii:
Watu wakiwekwa hai katika mateso yasiyoisha, wakihudumiwa na mashetani
Je, maelezo haya yanasikika yakifahamika?
Ni makadirio makubwa ya Kuzimu… duniani
Ni mara ngapi tumejiuliza ulimwengu ungefanya nini ikiwa tungeonja hukumu ya Kuzimu?
Hapa kuna nafasi yetu ya kujua
Na hata idadi ya miezi ni uthibitisho kwamba hii ni ishara ya neema ya Mungu kwa wasioamini
Kwa sababu namba tano ni namba ya neema katika Maandiko Matakatifu
Lakini baada ya miezi mitano hukumu ya kwanza ya ole inafikia kikomo lakini nyingine mbili zinabaki