Imefundishwa na
Stephen Armstrong
Imefundishwa na
Stephen ArmstrongTayari tumeelewa na kupanga vizuri katikati ya Dhiki Kuu, sasa ni wakati wa kuondoka katika kipindi hiki na kuingia katika miezi na majuma ya mwisho ya ile miaka saba.
Tunapofanya hivyo, hebu tupitie haraka mahali ambapo dunia imesimama katika hatua hii
Shetani amemfufua Mpinga Kristo, na anakaa ndani ya mwili wake
Kwa nguvu za Shetani, Mpinga Kristo anatawala ulimwengu, akisherehekewa kama Masihi na Mwokozi
Shetani amemwinua nabii wa uongo kuongoza ulimwengu katika dini mpya inayomwabudu Mpinga Kristo
Na sanamu isiyo ya kawaida imewekwa katika hekalu la Kiyahudi ili kuwakumbusha watu kuhusu mungu mpya wa ulimwengu
Ulimwengu umeitwa kumwabudu mungu huyu mpya, na wote wanachukua alama inayoonyesha nia yao ya kumwabudu
Kwa sehemu kubwa, wanaopinga ni wale wanaomwamini Yesu na Wayahudi wanaobaki kujitolea kwa Yahweh.
Miongoni mwa makundi haya, baadhi yako salama huko Petra
Wengine wako chini ya mateso kote ulimwenguni na hasa Yerusalemu
Na wengi huuawa kishahidi na kuingia Mbinguni kupumzika kutokana na majaribu haya na kusubiri ufufuo
Wakati huo huo, dunia inafurahia amani isiyotulia kwa sehemu kubwa ya nusu ya pili ya Dhiki
Hukumu za muhuri na hukumu za tarumbeta zimekuja na kutoweka katika miaka 3.5 ya kwanza.
Hukumu za bakuli bado zinasubiri, lakini haziji mara moja
Na kwa kuwa hukumu za bakuli ndizo kitendo kinachofuata katika tamthilia hii, simulizi ya kitabu inaruka kutoka katikati hadi mwisho wa miaka saba.
Na Sura ya 15 inatupeleka kwenye njia hiyo ikianza na ishara nyingine Mbinguni
Kwa mara nyingine tena, mawazo ya Yohana yanaelekezwa katika ulimwengu wa Mbinguni ili kushuhudia ishara nyingine kubwa na ya ajabu Mbinguni
Yohana anaita kile anachokiona ishara, alama ya mfano; kwa kweli, sura yote ya 15 ni ishara hiyo.
Sura nzima inatumia mfululizo wa alama ili kutoa hoja
Ishara inaanza na malaika saba wakiwa wameshika mabakuli saba
Yohana anasema mabakuli haya ndiyo ya mwisho, ikimaanisha hukumu ya mwisho ya Dhiki
Zaidi ya hayo, hizo ndizo hukumu za mwisho za Mungu kama inavyotakiwa chini ya Agano la Kale.
Kumbuka, kipindi cha Dhiki chenyewe ni matokeo ya masharti ya Agano la Kale kati ya Bwana na Israeli.
Yote yanayotokea katika kipindi hiki cha miaka saba yaliwekwa kwa ajili ya Israeli kulingana na agano hilo
Kama Danieli alivyoambiwa na Gabrieli
Na uteuzi huo ulikuwa kwa madhumuni ya kushughulikia dhambi za Israeli chini ya Agano la Kale.
Kwa hiyo wajibu wa Mungu wa kumimina ghadhabu juu ya Israeli chini ya masharti ya agano hilo utakamilika kwa hukumu hizi saba.
Kwa sababu hukumu hizi hazielekezwi kwa waumini, Bwana hutoa ulinzi kwa Wayahudi waaminio huko Botzrah
Lakini kwa Israeli iliyobaki, kumiminwa kwa ghadhabu ya Mungu kunawasafisha na kuwatakasa
Mungu hutumia hukumu kuwakatilia mbali baadhi katika Israeli huku akiwasafisha wengine
Hivyo ingawa Wayahudi wengi wasioamini wataangamia, wengine watakuja kwenye imani kupitia mchakato huo
Kwa kifupi, hicho ndicho tunachokiona kikitokea katika kipindi kilichobaki cha Dhiki Kuu
Mungu hupunguza umakini wake kwa Wayahudi wasioamini huku akileta hukumu dhidi ya adui na ulimwengu usioamini
Tukirudi kwenye Sura ya 15, hebu tuangalie ishara ya Yohana:
Ishara hiyo ina sehemu nyingi, ikianza na bahari ya kioo iliyochanganywa na moto
Ni wazi kwamba bahari, kioo na moto kwa kawaida havichanganyiki vizuri
Tunapaswa kufahamu kwamba Yohana anajaribu kuelezea tukio bila marejeleo
Kwa hiyo anarejelea vipengele anavyovijua kutoka duniani na kuvichanganya katika michanganyiko isiyowezekana
Ni wazi kwamba anaona kitu cha ulimwengu mwingine
Wale waliosimama juu ya "bahari" hii ni wale waliomshinda mnyama, jambo linalorejelea wale waliouawa kwa ajili ya imani yao wakati wa Dhiki Kuu.
Kifo chao kinaitwa "ushindi" juu ya mnyama na sanamu yake na namba ya jina lake
Kifo ni ushindi kwa sababu humwondoa mtu kutoka kwenye ushawishi wa mnyama na kumleta mahali pa kupumzika.
Mara tu mtakatifu anapokufa katika Dhiki, hupita kutoka utawala wa adui hadi utawala wa Bwana
Na kwa kuwa wameuacha ulimwengu nyuma, hawako tena karibu na adui ambaye ametupwa chini.
Walimshinda mnyama na alama, Yohana anasema, kwa maana kwamba hawakukubali kamwe madai yake ya kumwabudu au kupokea chapa (alama) yake.
Kufanya mambo haya kungewafanya wasipate nafasi ya kuwa na Bwana.
Kwa sababu wamekufa bila kukubali madai ya adui, wamefaulu mtihani na kuingia Mbinguni.
Nao waliishinda ile alama kwa sababu hawakuupenda uhai wao wa kimwili kuliko Bwana.
Huu ndio hasa mtazamo wa milele ambao waumini wote wanatarajiwa kuwa nao na kuudumisha.
Anayetafuta kupata uhai wake ataupoteza, na anayepoteza uhai wake atapata uzima wa milele.
Kisha, tunawaona watakatifu hawa wa Dhiki wakiimba kwa vinubi, wakiimba wimbo wa Musa na wimbo wa Mwanakondoo.
Hizi ni nyimbo mbili tofauti katika sura hii
Wimbo wa Mwanakondoo umerekodiwa hapa katika mstari wa 3-4, huku wimbo wa Musa ukirejelea wimbo wa awali kutoka Agano la Kale.
Maneno ya wimbo wa Mwanakondoo ni sifa kwa Yesu haswa
Haumtaji Yesu kamwe kwa jina, lakini tunajua inamzungumzia Yesu kwa sababu unaitwa wimbo wa “Mwanakondoo”
Waimbaji wanatangaza kwamba Yesu ndiye Mfalme mwenye haki wa mataifa
Hivi karibuni Mwana-Kondoo ataabudiwa na mataifa yote
Kauli hizi zinaonyesha kwamba Dhiki Kuu inakaribia kuisha hivi karibuni na kurudi kwa Yesu kunakaribia.
Waimbaji hawa pia wanaimba wimbo wa Musa, ambapo katika Maandiko Matakatifu kuna nyimbo mbili zinazowezekana kuwa miongoni
Uwezekano wa kwanza ni wimbo ulioimbwa na Musa katika Kumbukumbu la Torati 32
Musa anapokaribia kufa na taifa linaingia katika Nchi ya Ahadi bila yeye, anaonya kuhusu siku za kisasi ambapo Bwana atashughulikia dhambi yao
Katika siku zijazo, Israeli watakuwa wasioamini, wakiabudu miungu mingine na kumpuuza Mungu, Mwamba, aliyewaokoa.
Na matokeo yake, Bwana ataleta maafa juu ya watu wake na atakapoona nguvu zao zimepotea watavunjika moyo.
Anawashusha ili kuwavunja mioyo yao ya uasi
Wimbo huo ni wa kinabii waziwazi na utimilifu wake wa mwisho unapatikana katika matukio ya Dhiki
Kumbuka, uhusiano wao ulianzishwa kwa maagano
Agano moja lilianzisha uhusiano bila masharti, yaani Agano la Ibrahimu
Lakini agano jingine, Agano la Musa, liliwasili kando ya agano la kwanza, na lilikuwa na masharti.
Kutotii kwa Israeli agano hilo kulihitaji Mungu kumimina hukumu yake dhidi ya taifa hilo kwa ajili ya dhambi zao kulingana na masharti yake.
Kipindi cha historia ambacho Bwana analeta hukumu hizi kinaitwa Enzi ya Mataifa kulingana na kile tulichojifunza katika Danieli
Na Enzi ya Mataifa inafikia kilele chake kwa wakati wa Dhiki Kuu
Lakini kuna wimbo wa pili wa Musa katika Agano la Kale, na pia una umuhimu kwa wakati huu
Katika Kutoka 15:1-18 Musa anawaongoza watu wa Israeli katika wimbo wa sifa baada ya taifa kuokolewa kutoka kwa jeshi la Farao
Bwana alikuwa amefunga Bahari Nyekundu (pia hujulikana kama bahari ya Shamu) juu ya magari yaliyokuwa yakisonga mbele na kulizamisha jeshi
Wimbo huu pia ni picha ya kitakachotokea katika siku za mwisho
Kwa kweli, uzoefu mzima wa Kutoka ni picha ya Dhiki
Kutoka ni hadithi ya Israeli ikitoroka utumwa kwa kukimbia jangwani kutoka kwa adui aliyeazimia sana
Hatimaye kupitia hukumu za kimiujiza, Bwana anawaleta Israeli kwake ili wakae salama katika Nchi ya Ahadi
Kwa hiyo kwaya ya mbinguni inaimba wimbo wa Musa, ambao unaweza kuwa vipengele vya nyimbo hizi zote mbili za Agano la Kale, kwa sababu zote mbili zinahusiana.
Kwa upande mmoja, Bwana anatimiza ahadi yake ya kuleta kisasi na hukumu dhidi ya Israeli kwa ajili ya dhambi yao
Na kwa upande mwingine, atawaokoa watu wake kutoka kwa Mpinga Kristo mwishoni
Sura chache zinazofuata za Ufunuo zinaelezea jinsi Bwana anavyofanya hivyo
Kwa hiyo hebu tueleweshe tukio hili kwa kuelewa jinsi nyimbo hizi zilivyo "ishara"
Tuna tukio la mbinguni linaloelezea jambo fulani kuhusu kitakachotokea mwishoni mwa Dhiki kupitia nyimbo.
Wimbo wa kwanza ni wimbo unaomhusu Yesu unaoonyesha ni wimbo wa waamini ulioimbwa kwa waamini
Na wimbo huo unaonyesha kwamba kurudi kwa Kristo kumekaribia na wakati wake wa kutawala umekaribia
Yeye pekee ndiye mwenye haki na mtakatifu tofauti na madai ya kufuru ya adui duniani
Ishara hii kutoka Mbinguni itampa mwamini aliye katika Dhiki kitu cha kushikamana nacho wanapokabiliana na mateso makali huku wakitarajia mwisho.
Wakati huu huenda utahisi karibu na siku za wakristo waliokuwa wanatupwa na kulishwa kwa simba huko Roma.
Majeshi ya adui yatagawanya familia, kuwaua watoto mbele ya wazazi wao au wake zao mbele ya waume zao.
Na watafanya ukatili mkubwa zaidi kuliko ulimwengu ulivyowahi kujua
Lakini imani ya mwamini iko katika kujua kwamba wanamshinda adui kupitia kifo na Kristo atarudi kutawala hivi karibuni.
Lakini wimbo(nyimbo) wa Musa ni ishara kwa kundi tofauti kabisa katika nusu ya pili ya Dhiki
Nyimbo za Musa huimbwa kwa Wayahudi wa Dhiki, hasa kwa Wayahudi wa kawaida ambao bado hawajamwamini Yesu.
Sehemu ya kwanza ya wimbo kutoka Kumbukumbu la Torati inawakumbusha watu wa Mungu kwamba hukumu hii ni matokeo ya matakwa ya Agano la Kale
Bwana atawapitisha Israeli katika wakati wa hukumu na kuwafanya wapate udhaifu mkubwa
Kupitia hukumu, taifa linapatanisha dhambi zao na Bwana anabaki mwaminifu kwa ahadi Zake za kuleta hukumu hiyo
Kwa kushangaza, wimbo wa Musa unawapa Israeli tumaini kwa sababu unasema kwamba matukio haya hayako nje ya udhibiti wa Mungu.
Mungu anabaki na udhibiti na anatimiza ahadi zake na ataleta matokeo mazuri mwishowe
Na kwa sababu hiyo hiyo, wimbo wa pili wa Musa kutoka kitabu cha Kutoka unawakumbusha Wayahudi hawa uaminifu wa Mungu katikati ya mashambulizi
Mambo yalipoonekana kuwa mabaya zaidi kwa Israeli, Bwana aliwaokoa mwishoni
Kwa hiyo Israeli inaweza kuwa na ujasiri kwamba Bwana atawaangusha wale wanaoinuka dhidi ya watu wake
Baadaye mwishoni mwa Dhiki tutaona jinsi Bwana anavyotimiza ahadi hizi kwa Israeli katika siku ya kukata tamaa.
Kwa hiyo ishara ya Sura ya 15 ni kwa makundi mawili yanayoteswa katika nusu ya pili ya Dhiki
Waumini wanaambiwa watarajie kuja na kutawala kwa Bwana mwishoni mwa hukumu za bakuli
Na Wayahudi wa Orthodox wanaweza kutarajia wokovu wa Bwana kwa watu wake
Ujumbe huu ni faraja na kimasihi kwa wale walio duniani katika siku hizi.
Sehemu inayofuata ya ishara inaelekea hekaluni Mbinguni na kufunguliwa kwa hema la kukutania
Katika ulimwengu wa mbinguni kuna hema, sawa na ile ambayo Musa aliagizwa kuijenga kwa ajili ya Israeli katika Sheria.
Mwandishi wa Waebrania anatuambia kwamba hema ya duniani ambayo Bwana aliwapa Israeli ilifanana na toleo la mbinguni.
Katika hema la kukutania duniani kulikuwa na sanduku lenye kiti cha rehema, ambalo ni jina lililopewa sehemu ya juu au kifuniko cha sanduku.
Kwa hiyo tunadhania kwamba katika hema la mbinguni pia kuna kiti cha rehema
Na kwa kweli, Ezekieli 28 inatuambia kwamba mwanzoni Shetani alikuwa kerubi aliyelinda kiti cha rehema mbinguni.
Utukufu wa Mungu wa Shekina ulikaa katika hema la duniani ukifunika juu ya kiti cha rehema
Lakini katika hatua fulani katika historia ya Israeli, utukufu wa Bwana uliondoka hekaluni muda mfupi kabla ya Enzi ya Mataifa kuanza.
Na tangu Enzi hiyo ilipoanza, utukufu wa Bwana haujawahi kurudi kwa Israeli
Hautarudi, kulingana na Ezekieli, hadi Ufalme uanze na hekalu jipya lijengwe
Kwa hiyo sasa Bwana anapojiandaa kumimina ghadhabu yake ya mwisho juu ya Israeli na ulimwengu, anafungua hema la kukutania Mbinguni kama ishara
Utukufu wa Bwana juu ya kiti cha rehema unaonekana kwa muda ukimaanisha kurudi kwa Bwana kwenye hema la kukutania.
Hivi ndivyo Ezekieli alivyoona kuhusu siku hiyo iliyokuwa inakuja:
Kwa hiyo sehemu inayofuata ya ishara inaonyesha kwamba wakati wa Bwana kumaliza kwa ghadhabu na kurudi kukaa na Israeli umefika.
Na pamoja na hayo malaika wanaibuka wakiwa na mabakuli ya hukumu ya mwisho
Hukumu ya Tarumbeta ya saba ni hukumu za mabakuli saba, na sasa tunaona mabakuli hayo yakitayarishwa Mbinguni kwa hiyo tarumbeta ya mwisho iko karibu kupigwa.
Ghadhabu ya Mungu kwa kawaida huonyeshwa katika Maandiko kama kitu kilichomwagwa
Unaweza kupata mifano ya ghadhabu inayoonyeshwa kama kitu kilichomwagika kutoka kwenye kikombe au kilichonywewa kutoka kwenye kikombe.
Na ghadhabu au hukumu ya Mungu pia inasemekana kuhifadhiwa au kujazwa kikombe au chombo kingine.
Na sasa tunaona ghadhabu ikipimwa si katika vikombe bali katika mabakuli, ikionyesha aina kubwa zaidi ya hukumu hii.
Israeli imejiwekea ghadhabu na sasa itamwagwa kikamilifu
Kama Paulo alivyoandika katika Warumi
Kisha wakati wa kuvutia unatokea Mbinguni
Hekalu lilijaa moshi unaowakilisha utukufu na nguvu za Bwana, na kisha kila mtu alizuiliwa kuingia hekaluni
Ni nani kwa kawaida huingia hekaluni mwa Mungu? Katika kisa cha Israeli na Sheria, kuingia kulihusu makuhani pekee
Na katika kisa cha Patakatifu ambapo palikuwa na kiti cha rehema, ni Kuhani Mkuu pekee ndiye aliyeweza kuingia.
Kwa hiyo tukidhani kwamba hema ya mbinguni inafanya kazi kwa njia sawa, basi lazima tuhitimishe kwamba hakuna kuhani anayeingia hekaluni.
Ni kuhani gani anayeishi Mbinguni? Kuna mmoja tu: Yesu, Kuhani wetu Mkuu
Kwa hiyo dalili ni kwamba Baba amemzuia Yesu kuingia hekaluni hadi mwisho wa hukumu za mabakuli
Kama Yesu hawezi kuingia hekaluni, basi hawezi kwenda mbele za Baba kufanya maombezi
Na kama hawezi kufanya maombezi, basi hakuwezi kuwa na neema inayotolewa
Hii ni ishara zaidi kwamba hakuna imani mpya inayowezekana duniani hadi mwisho wa hukumu za bakuli
Kumbuka, Sura ya 15 ni sura ya mpito inayotuongoza kutoka katikati ya Dhiki
Na kwa hiyo, inatuambia jinsi nusu ya pili ya Dhiki itakavyokuwa
Hukumu za mabakuli zitafanyika karibu na mwisho wa wakati huu, na hadi zitakapomalizika, hakuna fursa ya imani duniani.
Sasa tukiwa mwisho wa Sura ya 15 tunaondoka rasmi katikati ya miaka saba ya Dhiki na tukiwa na Sura ya 16 tunaelekea kwenye wiki za mwisho.
Kama ilivyo katikati ya Dhiki, mwisho wa miaka saba unahusisha seti tata ya matukio yanayoingiliana
Kwa hiyo tunapojifunza sura hizi, tunaendelea kujenga uelewa wetu kwa kutumia grafu na michoro.
Tutaelezea matukio kwa mfuatano na kuelewa chanzo na athari zake zote.
Tuanze na hukumu tano za kwanza za bakuli zinazoanza kipindi hiki cha mwisho cha Dhiki
Ghadhabu ya mwisho ya Mungu iliyomwagwa huleta kiwango kipya cha mateso na taabu duniani
Kwanza, Mungu huondoa faraja ya kimwili ya mwanadamu kwa vidonda vichafu
Loathsome linatokana na neno la Kigiriki linalomaanisha mchafu na mwenye uovu (kwa kweli kiuhalisia ni neno la maana ya uovu au mabaya)
Ikiwa vidonda hivi ni vichafu au viovu, lazima viharibu mwili kwa njia zisizofikirika
Hebu fikiria kitu kilicho kama vile jinsi mwili wa Yesu ulivyoraruliwa vipande vipande kwa kupigwa kwake
Pili, Mungu anakomesha viumbe vyote vya baharini kwa kuzigeuza bahari zote kuwa damu
Mbali na idadi isiyohesabika ya samaki waliokufa na kuoza, damu yenyewe ingeanza kuganda na kuoza.
Hii pia ingezuia mzunguko wa maji wa sayari na kuzuia mvua yote
Na pia itasababisha janga lisilowezekana la kimazingira na kufanya usafiri baharini usiwezekane
Hii inafuatiwa na bakuli la tatu na kufanya vyanzo vya maji safi pia kugeuka kuwa damu
Malaika anaeleza kwamba damu ya hukumu hizi ni malipo kwa ulimwengu unaomwaga damu ya watakatifu
Na kwa hiyo, malaika anatangaza kwamba ulimwengu unastahili kuwa bila maji
Hukumu hii ni mojawapo ya dalili nyingi kwamba hukumu za mabakuli hutokea mwishoni kabisa mwa miaka saba.
Mtu anaweza kuishi kwa muda gani bila maji ya kunywa? Siku chache tu
Labda dunia itaishi kwa akiba ya maji ambayo inaweza kuongeza muda wa kuishi kwa muda, lakini hakika si kwa miaka mingi.
Nne, jua huongezeka ghafla kwa nguvu kiasi kwamba huwachoma wanadamu
Hebu fikiria kuishi na vidonda viovu katika ulimwengu usio na mvua (kwa sababu bahari ni damu) na hakuna vyanzo vya asili vya maji safi.
Sasa ongeza kwenye hilo jua kali linalotoa ndimi za moto zinazounguza dunia na watu.
Joto hilo pia lingeongeza kiwango cha kuoza kwa wanyama waliokufa kila mahali na kufanya hewa kuwa duni.
Hatimaye, bakuli la tano linaitupa dunia gizani na giza ni kali sana kiasi kwamba husababisha maumivu yasiyovumilika
Giza husababisha maumivu vipi?
Sio tu ukosefu wa nuru ya kimwili...ni giza la kiroho
Kama vile Baba alivyoondoa uwepo Wake kutoka kwa Yesu alipokuwa akining'inia msalabani, Bwana ameuacha ulimwengu wazi
Kwa kuwa uumbaji wa Mungu umetenganishwa na Muumba wake, umeachwa chini ya rehema ya nguvu za kiroho za giza
Kwa hiyo kwa muda, ulimwengu unahisi athari ya ghadhabu ya Bwana kwa kupitia ukosefu wa ulinzi wake.
Huenda umegundua mpangilio unaojulikana katika hukumu hizi nyingi
Joto kali, giza, hakuna maji, hakuna kiburudisho, chini ya rehema ya adui, hakuna unafuu kutokana na mateso ya kimwili
Ulimwengu unapitia hakikisho la Jehanamu, kwa sababu wanavumilia ghadhabu ya Mungu
Kuzimu yenyewe ni mahali ambapo ghadhabu ya Mungu humwagwa kila mara
Kwa hiyo inaeleweka kwamba ghadhabu Yake iliyomwagwa ingehisiwa kwa njia kama hizo
Mwitikio wa ulimwengu kwa majanga haya katika mst.9 ni kuendelea kumkufuru Mungu bila toba.
Asili ya dhambi ya mtu asiyeamini ni ya milele na hivyo uasi wake utakuwa wa milele isipokuwa Mungu abadilishe asili yake.
Hivyo, kwa sababu hiyo hiyo adhabu ya asiyeamini lazima iwe ya milele pia
Hukumu hizi zinaimarisha ishara ya Sura ya 15 waliposikia wimbo wa Musa
Katika kitabu cha Kutoka, taifa la Misri liliwaweka Israeli mateka kwa hiyo Bwana alitumia hukumu kuwaweka huru watu wake
Hapa tena, taifa la Israeli limetekwa na adui, na Bwana anamimina hukumu ili kuwaweka huru watu wake
Hasa, bakuli la 1, 2, 3, na 5 zote zina ulinganifu katika Kutoka
Uhusiano huu ni wa makusudi, kwa sababu unatukumbusha kwamba hukumu hizi hatimaye zinawaletea watu Wake matokeo mema.
Mwishowe, hukumu za Kutoka ziliwaletea Israeli uhuru na hatimaye kuingia katika Nchi ya Ahadi
Vivyo hivyo, hukumu hizi ni sehemu ya mpango wa kuwakomboa Israeli kutoka utumwani mwa dhambi na kutokuamini na kuingia katika Ufalme.
Kwa hiyo sasa, kwa kuwa tumejifunza mabakuli matano ya kwanza, hebu tusimame ili tuangalie jinsi hukumu za mabakuli zinavyoingia katika mpango mzima wa mwisho wa Dhiki
Hukumu tano za kwanza ni uwasilishaji ama utoaji wa kimfumo wa Kuzimu duniani kwa ajili ya maandalizi ya kurudi kwa Bwana.
Tunaweza kuziita hukumu hizi kwa pamoja mapigo, kwa kutambua jinsi zinavyoakisi kitabu cha Kutoka
Zinatumika kuleta ghadhabu ya Mungu kwa ulimwengu, lakini pia ni maandalizi na mandhari kwa ajili ya matukio ya Sura ya 17 na 18.
Kisha tuna hukumu mbili za mwisho kuhusu hali ya hewa kabla ya kurudi kwa Kristo
Hukumu mbili za mwisho zinaweza kuonekana zisizo na maana ikilinganishwa na zile ambazo tayari tumeziona katika tano za kwanza
Lakini ni sehemu ya seti kubwa ya matukio
Tunaita kilele hiki Vita vya Har–Magedoni, na vina hatua nyingi
Vita hivi vinamaliza Dhiki Kuu na kusababisha Kuja kwa Pili kwa Kristo
Na hatua mbili za kwanza za vita zinaanza na hukumu mbili za mwisho za mabakuli
Hata neno lenyewe "Har–Magedoni" linaweza kuleta dhana potofu na makisio au mawazo mbalimbali yasiyo sahihi.
Wakristo wengi wamesikia kuhusu vita hivi lakini wengi hawajui wakati wake au kusudi lake, sembuse maelezo yake
Na kama vita vingi, matukio halisi ya vita ni magumu na hayana maelezo rahisi.
Kuanzia na ukweli kwamba vita vya Har–Magedoni si pambano moja la kijeshi, bali ni mlolongo wa matukio yanayoendelea kwa wiki kadhaa.
Inafanyika katika mfululizo wa maeneo na inahusisha makundi na wahusika wengi tofauti
Kama kawaida, Ufunuo utatupa muhtasari mpana wa matukio ya vita na jinsi yanavyohusiana na hukumu za mabakuli.
Lakini vipengele muhimu vya hadithi viko nje ya Ufunuo katika vitabu vingine vya Biblia, hasa katika manabii wa Agano la Kale.
Kinachochanganya zaidi, maelezo ya vita yametawanywa katika Sura zote za 16-19
Sura hizi zinatoa suluhisho kwa baadhi ya mambo yasiyoeleweka katika kitabu cha Ufunuo na kumalizia mada kuu za Maandiko kuanzia kitabu cha Kwanza ya Mwanzo.
Hasa, Mungu anamhukumu na kumwondoa adui na ushawishi wake muhimu zaidi kwa wanadamu: Babeli
Babeli yenyewe ni mada ya ajabu na changamano inayohitaji maelezo makini
Tutachambua haya yote katika wiki zijazo, lakini kwanza tunahitaji kuanzisha uhusiano kati ya mabakuli na matukio ya vita hivi.
Tuanze pale tulipoishia katika Ufunuo 16, wakati wa kumiminwa kwa hukumu ya bakuli la sita
Malaika wa sita anapomimina bakuli lake, tunaambiwa kwamba mto mkubwa, Frati, umekauka
Mto Frati ndio mto mkuu wa Mesopotamia katika Iraq ya leo unaopita karibu na mji wa kale wa Babeli
Tunajua kutokana na hukumu za awali za mabakuli kwamba mito yote ya Dunia imegeuzwa kuwa damu
Kwa hiyo mto huu ulikuwa tayari umebadilika na kuwa damu pia
Lakini damu yenyewe kwa sehemu kubwa ni maji, kwa hiyo bado ni sahihi kusema kwamba hukumu hii "imekauka" kutokana na hukumu hii ya bakuli.
Kwa kawaida, tunajiuliza ni vipi kukauka kwa mto (ikiwa tayari umegeuka kuwa damu) kunachukuliwa kama hukumu?
Katika mstari wa 12 tunaambiwa sababu: inawapa wafalme wa mashariki njia inayowezekana
Wafalme ni marejeleo ya Mpinga Kristo na wafalme saba wanaomtumikia katika siku hizi
Tunajua kutoka kwa Danieli kwamba Dhiki huanza na wafalme kumi pekee walio madarakani, ambao huwa saba wakati Mpinga Kristo anapoinuka kuwa kwenye mamlaka.
Kwa hiyo wafalme hao ndio wafalme wale wale walioelezwa hapa na mto unakauka ili kuandaa njia kwa ajili ya wafalme hawa saba wa dunia.
Mstari wa 12 unaposema “itengenezwe njia,” unazungumzia kufanya usafiri au mwendo uwezekane kwa wafalme
Ni wazi kwamba Bwana ndiye anayetekeleza hukumu hizi na kwa hiyo ndiye anayeandaa safari yao
Lakini kwa nini Bwana anataka wasafiri na hiyo ni hukumu gani?
Katika mstari wa 13-16 tunaanza kuona jinsi harakati hii inavyochangia katika hukumu za Mungu
Joka, mnyama na nabii wa uongo wanaona fursa wakati mto unapokauka ili kutekeleza mpango wa kumpinga Mungu
Wanatuma pepo wachafu kama wajumbe kwa wafalme wa dunia
Roho wasio safi ni pepo, na zinaelezewa kama vyura, ambayo ni ishara ya Agano la Kale kwa roho wasio safi
Mashetani huwaita wafalme saba wa dunia kukusanya majeshi yao ili kujiandaa kwa vita kubwa dhidi ya Mungu
Mahali pa kukusanyika kwa majeshi haya ni mahali panapoitwa kwa jina la Kiebrania, Har-Megiddo
Neno "Har" kwa Kiebrania ni kilima au mlima na "Megido" ni jina la mji kaskazini mwa Israeli katika Bonde la Yezreeli.
Kwa hiyo, kilima cha Megido ni Har-Megido kwa Kiebrania
Na katika tafsiri ya Kiebrania hadi Kiingereza, tunafika Har–Magedoni
Hapa ndipo wafalme hawa watakusanya majeshi yao kwa ajili ya vita vikubwa dhidi ya Mungu.
Vita hivyo tunavyokaribia kujifunza vinapata jina lake kutokana na mji huu na vita vinavyoanza katika eneo hili.
Kwa nini Shetani anawaita wafalme wa Dunia wakusanyike huko Har-Megido?
Na kwa nini Bwana anatumia hukumu ya bakuli la sita ili kuwezesha hili?
Kwanza, kumbuka uharibifu wa ajabu ulioletwa duniani na hukumu za mabakuli matano ya kwanza
Maisha duniani sasa karibu hayavumiliki na hayafai kuishi, na wale waliochukua alama ya mnyama wanaona kwamba muda wao ni mfupi.
Kama Shetani alipotupwa chini, ulimwengu kwa ujumla unatambua kwamba bila maji kifo kiko karibu sana
Na wanajua kwamba Mungu ndiye anayehusika na hukumu hizi
Kwa hiyo Shetani, ambaye pia anajua wakati wake ni mfupi, anaamua kwamba lazima ajiandae kumwangamiza Kristo wakati wa kurudi kwake.
Kwa hiyo kwa ushawishi wa Mpinga Kristo na nabii wa uongo, Shetani anaita ulimwengu kupigana kama kitu kimoja dhidi ya Kristo
Huenda anazungumzia hali ya dharura ya dunia na kutangaza hii kama tumaini pekee la kuishi.
Kwa hiyo, Shetani na ulimwengu wakiwa katika mashua moja, wote wakitafuta njia ya kumshinda Mungu na kuepuka kifo, walianza kwenda vitani.
Kwa hiyo wito unatolewa kwa majeshi ya Mpinga Kristo kukusanyika kaskazini mwa Israeli kwa ajili ya shambulio kubwa dhidi ya mji wa Bwana.
Ili Bwana atakaporudi kwenye Mlima wa Mizeituni na hekaluni, majeshi ya Mpinga Kristo yatakuwa yakimngojea kumwangamiza.
Zaidi ya hayo, adui atawalenga Wayahudi waliobaki waliojificha mjini.
Na ikiwa ataweza kuwaangamiza Wayahudi hawa, anatumaini kufanya kurudi kwa Kristo kuwe jambo lisilowezekana
Vita hivi vitatokea katika hatua tano katika sura kadhaa zijazo, na ya kwanza kati ya hatua hizo ni hukumu ya bakuli la sita
Hatua ya I ya vita vya Har-Magedoni ni harakati za majeshi ya Mpinga Kristo kutoka katika mji wake mkuu na kuelekea Israeli.
Hatujasikia jina la mji mkuu wa Mpinga Kristo bado, lakini kukauka kwa mto Frati kunatupa kidokezo
Mji wa Babeli uko upande wa mashariki wa mto huo, huku Israeli ikiwa upande wa magharibi
Kwa hiyo vikosi vinavyoelekea Israeli vingehitaji mto ukauke
Tutaona uthibitisho kwamba Babeli ndiyo makao yake makuu baadaye katika Ufunuo
Mto ulikuwa kikwazo kwa harakati zake kuelekea magharibi hadi Yerusalemu, hasa katika hali yake ya damu.
Kwa hiyo Bwana anakausha mto ili kuwezesha harakati
Na mapepo huitikia hatua ya Mungu kwa kuwaita wafalme kwenda Har-Megido
Hii ni hukumu kwa sababu inaanzisha vita ambayo hatimaye huleta kifo kwa wasioamini wote na kushindwa kwa Shetani na Mpinga Kristo.
Kwa hiyo majeshi ya dunia yanahama kutoka Babeli kuelekea magharibi hadi yanapokusanyika karibu na Har-Megido
Majeshi hutumia eneo hili kama mahali pa maandalizi kwa ajili ya vita
Vita halisi vitafanyika katika maeneo mengine mawili
Na mbali na vita hivyo, Bwana anaanzisha uharibifu katika eneo la tatu.
Hatimaye, katika mst.15 Bwana anaweka kauli ya mabano kwa mwamini anayeishi katika siku hizi ngumu za mwisho.
Mapema katika Ufunuo 3 katika barua yake kwa Laodikia, Bwana alilionya kanisa kuwa tayari kwa ajili ya Unyakuo
Angekuja bila kutarajia na ni waaminio pekee ndio wangepokelewa Mbinguni
Kwa hiyo Yesu aliwaambia wasioamini kanisani wawe tayari kwa sababu hawangejua saa ya kuja kwake.
Hutapata nafasi ya kurekebisha uhusiano wako na Mungu kwa dakika za mwisho kwa sababu hutaona dakika hiyo ikija.
Vivyo hivyo, ulimwengu hautatambua kwamba Kuja kwa Pili kwa Yesu kumekaribia
Na kwa hiyo lazima wajue na kuamini kabla ya siku hiyo kufika
Ni tatizo lile lile lakini kwa wakati tofauti
Na bado wito ni ule ule…amini wakati leo bado inaitwa “leo”